Mheshimiwa anacheza ngoma kitamaduni

“Ninahisi kuheshimiwa sana leo,” Koti kubwa akasema kwa wale wanaofanya sherehe ya kumkaribisha kimila. “Na ninajua unamheshimu nani. Nitawafanyia mambo mengi ya ajabu.”

Koti Kubwa alikuwa amerudi kutoka kwenye ziara na kujivunia kuhusu safari zake za ajabu. Alizungumza kwa kirefu kuhusu watu mbalimbali aliokutana nao na mambo yake ya ajabu yaliyomletea umaarufu na sifa kutoka kwa watu kila mahali.