“Tucheze kwa haki,” alisema Kapteni wa Timu Punda.
“Ndiyo, mshindi apatikane kwa juhudi,” akajibu Kapteni wa Timu Tumbili.
Ndovu akapuliza kipenga chake kwa nguvu—fiiiiiiii! Mechi ikaanza.
Ndege walikusanyika kwa shangwe, kila mmoja akiwa na matumaini ya kuboresha maisha yao. Miongoni mwao alikuwa bata, ambaye alipenda kula kuliko kitu chochote kingine.